Ruka kwenda kwenye maudhui makuu

Ukurasa ulisasishwa mwisho: 18 Oktoba 2025

Jinsi ya kutumia pochi

Pata maelezo ya jinsi ya kutumia vipengele vyote vya msingi vya pochi. Ikiwa bado huna, angalia Jinsi ya kuunda akaunti ya Ethereum.

Fungua pochi yako

Unapaswa kuona dashibodi ambayo itaonyesha salio lako na iwe na vitufe vya kutuma na kupokea tokeni.

Pokea sarafu za kidikitali

Je! ungependa kupokea sarafu ya kidigitali kwenye pochi yako?

Kila akaunti ya Ethereum ina anwani yake ya kupokea ambayo ni mlolongo wa kipekee wa nambari na barua. Anwani hufanya kazi kama nambari ya akaunti ya benki. Anwani za Ethereum zitaanza na "0x" kila wakati. “Unaweza kushirikisha anwani hii na mtu yeyote: ni salama kufanya hivyo.”

Anwani yako ni kama anwani yako ya nyumbani: unahitaji kuwaambia watu ni nini ili wakupate. “Ni salama kufanya hivi, kwa sababu bado unaweza kufunga mlango wako wa mbele kwa ufunguo mwingine unaoudhibiti wewe pekee ili asiweze kuingia mtu yeyote, hata kama anajua unapoishi.”

Unahitaji kumpa yeyote anayetaka kukutumia pesa na anwani yako ya umma. Programu nyingi za pochi hukuruhusu kunakili anwani yako au kuonyesha msimbo wa QR ili kuchanganua kwa matumizi rahisi. “Epuka kuandika anwani yoyote ya Ethereum kwa mkono.” Hii inaweza kusababisha makosa ya ukarani kwa urahisi na kupoteza pesa.

“Programu tofauti zinaweza kutofautiana au kutumia lugha tofauti, lakini zinapaswa kukuongoza kupitia mchakato unaofanana ikiwa unajaribu kuhamisha fedha.”

  1. Fungua programu yako ya pochi.
  2. “Bofya kwenye ‘Pokea’ (au chaguo linalofanana nalo kwa maneno).”
  3. Nakili anwani yako ya Ethereum kwenye ubao wa kunakili.
  4. Mpe mtumaji anwani yako ya kupokea ya Ethereum.

Tuma sarafu ya kidigitali

Je, ungependa kutuma ETH kwa pochi nyingine?

  1. Fungua programu yako ya pochi.
  2. Pata anwani ya kupokea na uhakikishe kuwa umeunganishwa kwenye mtandao sawa na mpokeaji.
  3. Weka anwani ya kupokea au changanua msimbo wa QR ukitumia kamera yako ili usilazimike kuandika anwani kwa mkono.
  4. Bofya kwenye kitufe cha "Tuma" kwenye pochi yako (au njia mbadala iliyo na maneno sawa).

Uga wa kutuma kwa anwani ya sarafu ya kidigitali

  1. “Mali nyingi, kama DAI au USDC, zipo kwenye mitandao mbalimbali.” Wakati wa kuhamisha tokeni za sarafu za kidigitali, hakikisha kwamba mpokeaji anatumia mtandao sawa na wewe, kwa kuwa hizi hazibadilishwi.
  2. Hakikisha kuwa pochi yako ina ETH ya kutosha kulipia ada ya muamala, ambayo inatofautiana kulingana na hali ya mtandao. Pochi nyingi zitaongeza kiotomatiki ada iliyopendekezwa kwenye shughuli ambayo unaweza kuthibitisha.
  3. Muamala wako ukishachakatwa, kiasi kinacholingana cha sarafu ya kidigitali kitaonekana kwenye akaunti ya mpokeaji. Hii inaweza kuchukua popote kutoka sekunde chache hadi dakika chache kulingana na kiasi gani mtandao unatumika kwa sasa.

Kuunganisha kwa miradi

Anwani yako itakuwa sawa katika miradi yote ya Ethereum. Huhitaji kujiandikisha kibinafsi kwenye mradi wowote. Mara tu ukiwa na pochi, unaweza kuunganisha kwenye mradi wowote wa Ethereum bila maelezo yoyote ya ziada. Hakuna barua pepe au taarifa nyingine yoyote ya kibinafsi inahitajika.

  1. Tembelea tovuti ya mradi wowote.
  2. Ikiwa ukurasa wa mwanzo wa mradi ni maelezo tuli ya mradi, unapaswa kubofya kitufe cha "Fungua Programu" kwenye menyu ambayo itakuelekeza hadi kwenye programu halisi ya wavuti.
  3. “Mara tu ukiwa kwenye programu, bofya kwenye ‘Unganisha’.”

Kitufe kinachomruhusu mtumiaji kuunganisha kwenye tovuti kwa kutumia mkoba

  1. “Chagua pochi yako kutoka kwenye orodha ya chaguo zilizotolewa.” Ikiwa huwezi kuona pochi yako, inaweza kufichwa chini ya chaguo la "muunganisho wa pochi".

Kuchagua kutoka kwenye orodha ya mikoba ya kuunganisha nayo

  1. Thibitisha ombi la saini kwenye pochi yako ili kubaini muunganisho. Kusaini ujumbe huu hakupaswi kuhitaji kutumia ETH yoyote.
  2. Ni hayo tu! Anza kutumia programu. Unaweza kupata baadhi ya miradi ya kuvutia kwenye ukurasa wetu wa mfumo mtawanyo wa kimamlaka.

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara

Ikiwa ninamiliki anwani ya ETH, nawezaje miliki anwani sawa kwenye blockchain zingine?

“Unaweza kutumia anwani ile ile kwenye kiambajengo zote zinazolingana na EVM (ikiwa una pochi ya aina iliyo na kifungu cha urejeshaji.” Hii orodha (opens in a new tab) itakuonyesha minyororo ya bloku ambazo unaweza kutumia na anwani sawa. Baadhi mlolongo wa vitalu, kama Bitcoin, kutekeleza seti tofauti kabisa ya Mtandao Kanuni na unahitaji anwani tofauti na muundo tofauti. Ikiwa una mkoba mzuri wa mkataba unapaswa kuangalia tovuti ya bidhaa zake kwa maelezo zaidi kuhusu viambajengo vinazotumika.

Je, ninaweza kutumia anwani ileile kwenye vifaa vingi?

“Ndiyo, unaweza kutumia anwani ile ile kwenye vifaa vingi. Pochi kitaalamu ni kiolesura cha kukuonyesha salio lako na kufanya miamala, akaunti yako haihifadhiwi ndani ya pochi, bali kwenye kiambajengo.

Sijapokea sarafu ya kidigitali, ni wapi ninaweza kuangalia hali ya muamala?

Unaweza kutumia wachunguzi wa bloku kuona hali ya muamala wowote kwa wakati halisi. Unachohitaji kufanya ni kutafuta anwani ya pochi yako au kitambulisho cha muamala.

Je, ninaweza kufuta au kurejesha miamala?

“Hapana, mara tu muamala unapo thibitishwa, huwezi kuufuta.”

Ukurasa ulihaririwa mwisho: 18 Oktoba 2025

Je! makala haya yamekusaidia?